Monday, January 25, 2016

HII HAPA TAARIFA YA MAHAKAMA YA MWANZA KUHUSU HUKUMU YA ESTHER BULAYA KUPINGWA UBUNGE




Uchaguzi Mkuu wa Wabunge, Madiwani na Rais wa Tanzania ulifanyika October 25 2015, baada ya hapo matokeo yakatoka na kukawa na stori mfululizo kuhusu ishu ya matokeo ikiwemo Wabunge wengine waliofungua kesi Mahakamani kupinga matokeo.

Mmoja ya Wabunge ambao walifunguliwa kesi za kupingwa Ubunge Mbunge wa Bunda,Ester Bulaya nae alikuwa na kesi iliyofunguliwa Mahakama Kuu kanda ya Mwanza.

Kwanza ni kwamba Mahakama hiyo imefuta kesi hiyo, kingine ni kwamba Mahakama hiyo imesema waliofungua kesi hiyo ni wapigakura ambao hawana mamlaka ya kufungua kesi ya aina hiyo.
Source;Millardayo.

Thursday, November 19, 2015

HUYU HAPA WAZIRI MKUU ALIYETEULIWA NA RAIS JPM LEO.

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Serikali ya


Dar es Salaam.
Rais John Magufuli leo amewasilisha bungeni jina la Mbunge wa Ruangwa, Kassim Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya awamu ya tano.


Spika wa Bunge, Job Ndugai alipokea barua iliyotoka kwa Rais Magufuli kupitia kwa watumishi wa chombo hicho cha kutunga sheria na baada ya kuifungua ndipo aliposoma ujumbe huo uliotaja jina la Majaliwa ambaye alikuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali ya Mitaa (Tamisemi) anayeshughulikia elimu.


Baada ya tangazo hilo ambalo lilipokelewa kwa shangwe na wabunge wengi, Spika Ndugai aliahirisha bunge kwa dakika arobaini na tano kuwapa nafasi wabunge kutafakari uteuzi huo kisha kumthibitisha bunge litakaporejea.


Waziri Mkuu huyo mteule alizaliwa Disemba 22, 1960 na kupata elimu katika Shule ya Msingi Mnacho kati ya mwaka 1970-1976 kabla ya kujiunga na shule ya sekondari ya Kigonsera kati ya mwaka 1977- 1980.


Mwaka 1991-1993 alijiunga na Chuo Cha Ualimu Mtwara. Alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1994 na kuhitimu mwaka 1998 kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu cha Stockholm nchini Sweden kwa masomo ya juu.


Amehudumu katika nafasi mbalimbali tangu mwaka 1984 alipojiunga na utumishi wa umma kama mwalimu mkoani Lindi, Katibu wa Chama cha Waalimu Wilaya, Katibu chama waalimu Mkoa na Mkuu wa Wilaya.


Mwaka 2010 alichaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Ruangwa mkoani Lindi kabla ya Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete kumteua mwaka 2012 kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali ya Mitaa (Tamisemi) anayeshughulikia elimu.

Friday, August 21, 2015

KIKOSI KIPYA CHA WACHEZAJI WALIOITWA TAIFA STARS.



Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars  Charles Boniface Mkwasa August 21 ametangaza kikosi cha wachezaji 22 watakaosafiri kwenda kuweka kambi ya siku 8 Istanbul UturukiMkwasa ametangaza kikosi hicho ambacho kila mchezaji aliyeitwa anatakiwa kuripoti saa 5 asubuhi siku ya Jumapili August 23 tayari kwa safari usiku wake.
Taifa Stars inakwenda kuweka kambi Uturuki kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya kuwania kucheza AFCON 2017, mechi ambayo itachezwa Septemba 5 Uwanja wa Taifa Dar Es Salaam, orodha hiyo ya wachezaji 22 imetangazwa kutoka katika kikosi cha awali kilichotangazwa wiki mbili mbili nyuma.
Wachezaji walioitwa ni:
All Mustafa (Yanga SC)
Aishi Manula (Azam FC)
Said Mohamed (Mtibwa Sugar)
Shomari Kapombe (Azam FC)
Abdi Banda (Simba SC)
Mohamed Hussein (Simba SC)
Hassan Isihaka (Simba SC)
Juma Abdul (Yanga SC).
Haji Mngwali (Yanga SC).
Kelvin Yondani (Yanga SC).
Nadir Haroub (Yanga SC).
Mudathir Yahya (Azam FC)
Himid Mao (Azam FC)
Frank Domayo (Azam FC)
Salum Telela (Yanga SC)
Deus Kaseke (Yanga SC)
Said Ndemla (Simba SC)
John Bocco (Azam FC)
Farid Musa (Azam FC)
Rashid Mandawa (Mwadui FC)
Simon Msuva (Yanga SC)
Ibrahim Ajib (Simba SC.

Sunday, August 16, 2015

HII NI NYINGINE TENA KUHUSU LOWASSA NA WAFUASI WA UKAWA.

Jeshi la polisi jiji Mwanza limetumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa vyama vinavyounda ukawa ili wasiandamane kwenda uwanja wa ndege wa Mwanza kumpokea mgombea urais kupitia Chadema, Edward Lowassa, anayetarajiwa kuwasili jijini huko kusaka wadhamini
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Charles mkumbo, amesema mabomu hayo yametumika ili kuwazuia wafuasi hao wasiweze kujazana uwanjani hapo na kusimamisha shughuli nyingine.

Saturday, August 1, 2015

MAELEZO YA NAPE NNAUYE KUHUSU KUCHUKULIWA KWAKE NA ASKARI WA TAKUKURU.


Gazeti la MWANANCHI limeandika HAPA kwamba Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amefafanua ishu yake ya kuchukuliwa na askari wa Takukuru kwa mahojiano muda mfupi baada ya kuchukua fedha benki huko Lindi.
Nape anayewania ubunge wa Jimbo la Mtama, jana mchana aliamriwa na maofisa wa Takukuru kufika ofisi zao baada ya kutoka kuchukua fedha benki ya NMB eneo la Misonobarini mkoa Lindi.
Ninadhani hawa jamaa walipotoshwa. Mimi nimekwenda zangu benki kuchukua fedha, lengo langu ni kuwalipa mawakala,” alisema Nape jana jioni alipopigiwa simu na Mwananchi kutoa ufafanuzi na akaongeza kwamba “Wakaja hawa jamaa, wakajitambulisha kuwa wanatoka Takukuru, wakaniuliza ‘mbona ninachukua fedha nyingi kipindi hiki?’ Nikawaambia ‘nakwenda kulipa mawakala, na fedha zenyewe ni hizi Sh3.6 milioni
‘Basi, tukatoka taratibu tukaenda ofisini kwao, ni karibu tu na benki. Wakanihoji hata haikumalizika nusu saa, niliwaambia nataka kulipa mawakala wangu, tena fedha zenyewe hazitoshi, wako zaidi ya 100′ – Nape Nnauye
Nape aliongeza kusema kuwa walimkamata na akawaambia kuwa yeye ni mwadilifu >>> “Halafu ninyi, mnaacha marushwa makubwa makubwa huko, watu wanahonga halafu mnamvizia Nape masikini kwa Sh3mil?,” alisema.
Nape alielezea kufadhaishwa na tukio hilo akidai kuwa limetengenezwa kwa ajili ya kumchafua hasa kwa kuwa leo kuna kura za maoni lakini akasema anaamini yeye ni msafi ambapo Kamanda wa Takukuru wa Mkoa wa Lindi, Stephen Chami alikiri kumhoji Nape lakini akasema walijiridhisha kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kulipa mawakala.

“Unajua tuna watu wetu, kwenye maeneo mbalimbali hasa kipindi hiki cha uchaguzi, tumeweka watu wetu maeneo mengi, tunataka kukomesha rushwa,”
Source-millardayo.

Wednesday, July 1, 2015

SALAMA JABIR AZUNGUMZA HAYA KUHUSU VIDEO MPYA YA ALIKIBA.


salama jj

Mtangazaji wa Mkazi na jaji wa mashindani ya vipaji Tanzania [bss] Salama J ametoa mtazamo wake kwa mahache kupitia twitter kuhusu video mpya ya Ali Kiba ‘Chekecha Cheketua’. Soma Twit zake hapa.

salama 1

Kiukwel mashabiki wa muziki wa Tanzania tuache propaganda na longolongo zisizo na maana! Video ni kali so Big up kwa ALLY SALEH KIBA!...

Saturday, May 23, 2015

YA NKURUNZIZA MWACHIE MWENYEWE BWANA! EBU MUONE APA!

nziza2

Burundi kwa sasa iko kwenye vichwa vingi vya habari kutokana na hali ya machafuko inayoendelea nchini humo baada ya Raisi Pierre Nkurunziza kutangaza kugombea tena uraisi awamu ya tatu mfululizo!

nziza

Jaribio la kutaka kumpindua madarakani wakati akiwa Tanzania lilifeli na sasa uamuzi uliofikiwa ni kuahirishwa kwa uchaguzi wa wabunge nchini humo.
      Jambo lingine lililowashangaza watu ni kuwa pamoja na hali ya machafuko inayoendelea nchini humo yeye ameonekana akiwa uwanjani akicheza mpira kwa raha zake.

nziza3

Pia inasemekana kwamba mtu mmoja amepigwa risasi na askari waliokuwa wakilinda usalama mjini bujumbura wakati maandamano yalipokuwa yakifanyika.

Tuesday, May 19, 2015

WATOTO 2 WAFA KANISANI KWA GWAJIMA.

Watoto wawili ambao ni ndugu wamefariki dunia katika kanisa la ufufuo na uzima,linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima jijini Dar es salaam.
Watoto hao walifariki baada ya kupigwa na shoti ya umeme wakiwa katika ibada juzi jumapili wakati watoto hao wakiwa na waumini wengine wakifuatilia ibada ya kufunga ndoa.
Inadaiwa kuwa watoto hao walipigwa na shoti baada ya kukanyaga nyaya za umeme wakati waumini waliponyanyuka kwenda kuwapokea maharusi wakati wakiingia kanisani hapo.
Baba mzazi wa watoto hao David Oturo ameonyesha hali ya wasiwasi ya kutokukubaliana na mazingira ya vifo vya watoto wake Sara mwenye miaka 10 naGudluck mwenye miaka minne na kusema ni vifo vya utatanishi.
Alisema siku hiyo kulikuwepo na watoto wengi waliokusanyika katika viwanja vya kanisa hilo lakini ni watoto wake waliofikwa na mauti hayo.
Aliongeza kuwa kabla ya kufikwa na mauti hayo majira ya mchana Sara aling’atwa na nyuki sehemu ya mguu ambao walitokea katika kanisa hilo gafla.
Alisema jioni ndipo watoto hao walipopigwa na shoti na baada ya kuangalia nyaya hizo hazikuwa zimechunika sehemu yoyote wala kuwa na dalili ya hitilafu.
Source;millardayo!

Saturday, May 2, 2015

ALI KIBA AVAMIWA NYUMBANI KWAKE JIJINI DAR.


IMG-20150502-WA0007
     

IMG-20150502-WA0002


IMG-20150502-WA0000


IMG-20150502-WA0001


IMG-20150502-WA0003

Usiku wa kuamkia leo msanii Ali Kiba akiwa nyumbani kwake Kunduchi jijini Dar-es-salaam, amevamiwa na kundi la watu wapatao 15 wanaodhaniwa kuwa ni majambazi.
Watu hao waliokuwa na silaha za aina tofauti yakiwemo mapanga,visu na silaha za moto walifanikiwa kuvunja milango na kuingia ndani kisha kuwadhuru baadhi ya ndugu wa ali kiba na kuiba mali pamoja na kila kitu walichoweza kubeba.
   Baada ya abdu kiba kuhojiwa alisema kwamba yeye alikuwa masaki, Ali akampigia simu kwamba kuna watu kama 15 hivi wamevamia nyumbani kwao. Waliovamia waliruka ukuta saa tisa za usiku, wakavunja mlango wa sebuleni, wakawakuta vijana wawili ambao wanaishi nao, waliwapiga na kuwalazimisha waoneshe chumba ambacho Ali kiba yupo. Wale vijana wakajibu kwamba ali hayupo wakauliza chumba chake wakaoneshwa chumba cha Abdu kiba. 
    Wameingia chumbani wakamkosa Ali kiba, wameiba vitu vingi vya sebuleni na chumbani pia pamoja na pesa milion 2 na nusu zilizokuwa chumbani kwa Abdu kiba.
Abdu kiba akatoa taarifa polisi, wakafika usiku huo huo na kuanza ukaguzi eneo lote la nyumba,
Da! inasikitisha sana kwa taarifa hizi!..

Sunday, April 26, 2015

MO MUSIC - NITAZOEA NEW MP3 DOWNLOAD.


                                               
                                                        Mo music-Nitazoea mp3

                                          Download

Sunday, April 12, 2015

HII NDIO HALI HALISI YA VITAMBULISHO VYA UTAIFA MOROGORO





Na hivi ndivyo mambo yanavyoendelea mkoani Morogoro ambapo wanafunzi wa chuo kikuu cha SUA Morogoro wapo katika harakati za kufuatilia vitambulisho vya utaifa kutoka NIDA. Katika suala hili kumekuwa na changamoto mbalimbali kama vile kukosekana kwa elimu ya kutosha kuhusu namna ya kujaza fomu kwa usahihi na mambo mengine kama kukaa kwenye foleni kwa muda mrefu mpaka mtu uje upate kitambulisho hicho.
Baada ya kuzungumza na mmoja kati ya watu wa NIDA kuhusu changamoto ya kuwaelimisha watu kuhusu namna ya kujaza fomu hizo, Mheshimiwa huyo alisema kwamba watu inatakiwa wawaulize wengine wamejaza vipi hizo fomu au wanaweza kuitumia fomu ya mfano iliyobandikwa ili kufatisha namna ya kujaza vema hizo fomu.
Idadi ya wanafunzi ambao washafanikisha suala hilo ni ndogo ukilinganisha na idadi ya wanafunzi
waliopo chuoni hapo.Kwa sasa mambo yanaendelea vizuri na muda wa kufuatilia vitambulisho hivyo umeongezwa ili huduma hii iweze kutolewa kwa wote kama inavyotakiwa.

Sunday, March 8, 2015

JE UNALIFAHAMU HILI KUHUSU MZEE KIZITO WA SIRI YA MTUNGI?


Jina lake kamili anaitwa Nkwabi Ng'hangasamala. Ni msanii/muigizaji maarufu anayeng'ara sana katika  tamthilia ya SIRI YA MTUNGI. Watu wengi hawafahamu kwamba uyu mzee ni Professor wa chuo cha sanaa Bagamoyo. Ni mzee ambaye anajua kuuvaa uhusika pale anapokuwa anaigiza kiasi kwamba ameweza kuwavutia watu wengi kuifuatilia tamthilia hii ya siri ya mtungi ambayo hivi sasa ndio imefikia tamati.

Saturday, February 14, 2015

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014 HAYA HAPA!


 
       Tazama kwa urahisi matokeo ya kidato cha nne 2014 kupitia kingstar blog hapa!....


                                     Feb 14

                        Matokeo ya CSEE na QT 2014

 

Sunday, January 18, 2015

AVRIL FEAT OMMY DIMPOZ - HELLO BABY!


LYRICS/VERSE ZA WIMBO MPYA WA DIAMOND HIZI HAPA!.

Hizi hapa verse za wimbo mpya wa diamond platnumz - nasema nawe!

Verse 1
Hallooooooo!!!!!!
Mmmhh!! Aah, Kutwa viguru njiani majirani wote wamekuchokaaa...
Mara chumba cha fulani mtu gani we kwako usokaa
Washinda vibarazani ya wenzako kuropokaaa
Kwa kuwa umemuona Fulani ona usoo ulivyokukobokaaa
Sio mwisho vibaoni adi kwenye vigodoroo
Usio na haya usoni kote wazua migogoroo
Ivi wewe haujioni kuwa unakasoroo
Uso mchana jioni si wajuz si 2moro
Sio mwisho vibaoni kwenye vigodoroo
Usio na haya usoni kote wazua migogoroo
Ivi wewe haujioni kuwa unakasoroo
Uso mchana jioni si wajuz si aaaah!!!

Chorus
Nasema naweee x3
Uso haya nasema naweee
Umezoea (nasema naweee)
Chezea chezea (nasema nawee)
Aaah!! Umezidi (nasema naweee)
Zidi (nasema naweeee)
zidi (nasema naweee)
Verse 2
Mmmmmhhh, mmmh
Aahh!! Zingifuli zingifuli zinga mahala ukakaaa
Usoo mila desituri usiyejua tongozwa ukakataaa
Usio hiana fedhuri uongo umekujaaa
Kujifanya mashuhuri kumbe chaka umechakaa
Aagah!! Mwanzako mim turufu si garasa
Mwenye nyota ya umaarufu si kupapasa
Tena jokali la nguvu makarata
Lile hodari maguvu si kwasakwasa
Ooohh!!! Mwanzako mim turufu si garasa
Mwenye nyota ya umaarufu sio hozakosa
Chorus
Nasema naweee x3 (nawew nawe oohhhhhh)
Uso haya nasema naweee
Nasema naweee x 3(nawew oohhhhhh)
Nimechoka nasema nawee
Umezoea (nasema naweee)
Chezea chezea (nasema nawee)
Aaah!! Umezidi (nasema naweee)
Zidi (nasema naweeee)
Uso haya nasema naweee
Oooohhh!!! (nasema naweee)
Nasema nawee x 3 (nawew oohhhhhh)
Nimechoka nasema nawee….