Friday, August 21, 2015

KIKOSI KIPYA CHA WACHEZAJI WALIOITWA TAIFA STARS.



Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars  Charles Boniface Mkwasa August 21 ametangaza kikosi cha wachezaji 22 watakaosafiri kwenda kuweka kambi ya siku 8 Istanbul UturukiMkwasa ametangaza kikosi hicho ambacho kila mchezaji aliyeitwa anatakiwa kuripoti saa 5 asubuhi siku ya Jumapili August 23 tayari kwa safari usiku wake.
Taifa Stars inakwenda kuweka kambi Uturuki kwa ajili ya kujiandaa na mechi ya kuwania kucheza AFCON 2017, mechi ambayo itachezwa Septemba 5 Uwanja wa Taifa Dar Es Salaam, orodha hiyo ya wachezaji 22 imetangazwa kutoka katika kikosi cha awali kilichotangazwa wiki mbili mbili nyuma.
Wachezaji walioitwa ni:
All Mustafa (Yanga SC)
Aishi Manula (Azam FC)
Said Mohamed (Mtibwa Sugar)
Shomari Kapombe (Azam FC)
Abdi Banda (Simba SC)
Mohamed Hussein (Simba SC)
Hassan Isihaka (Simba SC)
Juma Abdul (Yanga SC).
Haji Mngwali (Yanga SC).
Kelvin Yondani (Yanga SC).
Nadir Haroub (Yanga SC).
Mudathir Yahya (Azam FC)
Himid Mao (Azam FC)
Frank Domayo (Azam FC)
Salum Telela (Yanga SC)
Deus Kaseke (Yanga SC)
Said Ndemla (Simba SC)
John Bocco (Azam FC)
Farid Musa (Azam FC)
Rashid Mandawa (Mwadui FC)
Simon Msuva (Yanga SC)
Ibrahim Ajib (Simba SC.

Sunday, August 16, 2015

HII NI NYINGINE TENA KUHUSU LOWASSA NA WAFUASI WA UKAWA.

Jeshi la polisi jiji Mwanza limetumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa vyama vinavyounda ukawa ili wasiandamane kwenda uwanja wa ndege wa Mwanza kumpokea mgombea urais kupitia Chadema, Edward Lowassa, anayetarajiwa kuwasili jijini huko kusaka wadhamini
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Charles mkumbo, amesema mabomu hayo yametumika ili kuwazuia wafuasi hao wasiweze kujazana uwanjani hapo na kusimamisha shughuli nyingine.

Saturday, August 1, 2015

MAELEZO YA NAPE NNAUYE KUHUSU KUCHUKULIWA KWAKE NA ASKARI WA TAKUKURU.


Gazeti la MWANANCHI limeandika HAPA kwamba Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amefafanua ishu yake ya kuchukuliwa na askari wa Takukuru kwa mahojiano muda mfupi baada ya kuchukua fedha benki huko Lindi.
Nape anayewania ubunge wa Jimbo la Mtama, jana mchana aliamriwa na maofisa wa Takukuru kufika ofisi zao baada ya kutoka kuchukua fedha benki ya NMB eneo la Misonobarini mkoa Lindi.
Ninadhani hawa jamaa walipotoshwa. Mimi nimekwenda zangu benki kuchukua fedha, lengo langu ni kuwalipa mawakala,” alisema Nape jana jioni alipopigiwa simu na Mwananchi kutoa ufafanuzi na akaongeza kwamba “Wakaja hawa jamaa, wakajitambulisha kuwa wanatoka Takukuru, wakaniuliza ‘mbona ninachukua fedha nyingi kipindi hiki?’ Nikawaambia ‘nakwenda kulipa mawakala, na fedha zenyewe ni hizi Sh3.6 milioni
‘Basi, tukatoka taratibu tukaenda ofisini kwao, ni karibu tu na benki. Wakanihoji hata haikumalizika nusu saa, niliwaambia nataka kulipa mawakala wangu, tena fedha zenyewe hazitoshi, wako zaidi ya 100′ – Nape Nnauye
Nape aliongeza kusema kuwa walimkamata na akawaambia kuwa yeye ni mwadilifu >>> “Halafu ninyi, mnaacha marushwa makubwa makubwa huko, watu wanahonga halafu mnamvizia Nape masikini kwa Sh3mil?,” alisema.
Nape alielezea kufadhaishwa na tukio hilo akidai kuwa limetengenezwa kwa ajili ya kumchafua hasa kwa kuwa leo kuna kura za maoni lakini akasema anaamini yeye ni msafi ambapo Kamanda wa Takukuru wa Mkoa wa Lindi, Stephen Chami alikiri kumhoji Nape lakini akasema walijiridhisha kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kulipa mawakala.

“Unajua tuna watu wetu, kwenye maeneo mbalimbali hasa kipindi hiki cha uchaguzi, tumeweka watu wetu maeneo mengi, tunataka kukomesha rushwa,”
Source-millardayo.

Wednesday, July 1, 2015

SALAMA JABIR AZUNGUMZA HAYA KUHUSU VIDEO MPYA YA ALIKIBA.


salama jj

Mtangazaji wa Mkazi na jaji wa mashindani ya vipaji Tanzania [bss] Salama J ametoa mtazamo wake kwa mahache kupitia twitter kuhusu video mpya ya Ali Kiba ‘Chekecha Cheketua’. Soma Twit zake hapa.

salama 1

Kiukwel mashabiki wa muziki wa Tanzania tuache propaganda na longolongo zisizo na maana! Video ni kali so Big up kwa ALLY SALEH KIBA!...

Saturday, May 23, 2015

YA NKURUNZIZA MWACHIE MWENYEWE BWANA! EBU MUONE APA!

nziza2

Burundi kwa sasa iko kwenye vichwa vingi vya habari kutokana na hali ya machafuko inayoendelea nchini humo baada ya Raisi Pierre Nkurunziza kutangaza kugombea tena uraisi awamu ya tatu mfululizo!

nziza

Jaribio la kutaka kumpindua madarakani wakati akiwa Tanzania lilifeli na sasa uamuzi uliofikiwa ni kuahirishwa kwa uchaguzi wa wabunge nchini humo.
      Jambo lingine lililowashangaza watu ni kuwa pamoja na hali ya machafuko inayoendelea nchini humo yeye ameonekana akiwa uwanjani akicheza mpira kwa raha zake.

nziza3

Pia inasemekana kwamba mtu mmoja amepigwa risasi na askari waliokuwa wakilinda usalama mjini bujumbura wakati maandamano yalipokuwa yakifanyika.

Tuesday, May 19, 2015

WATOTO 2 WAFA KANISANI KWA GWAJIMA.

Watoto wawili ambao ni ndugu wamefariki dunia katika kanisa la ufufuo na uzima,linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima jijini Dar es salaam.
Watoto hao walifariki baada ya kupigwa na shoti ya umeme wakiwa katika ibada juzi jumapili wakati watoto hao wakiwa na waumini wengine wakifuatilia ibada ya kufunga ndoa.
Inadaiwa kuwa watoto hao walipigwa na shoti baada ya kukanyaga nyaya za umeme wakati waumini waliponyanyuka kwenda kuwapokea maharusi wakati wakiingia kanisani hapo.
Baba mzazi wa watoto hao David Oturo ameonyesha hali ya wasiwasi ya kutokukubaliana na mazingira ya vifo vya watoto wake Sara mwenye miaka 10 naGudluck mwenye miaka minne na kusema ni vifo vya utatanishi.
Alisema siku hiyo kulikuwepo na watoto wengi waliokusanyika katika viwanja vya kanisa hilo lakini ni watoto wake waliofikwa na mauti hayo.
Aliongeza kuwa kabla ya kufikwa na mauti hayo majira ya mchana Sara aling’atwa na nyuki sehemu ya mguu ambao walitokea katika kanisa hilo gafla.
Alisema jioni ndipo watoto hao walipopigwa na shoti na baada ya kuangalia nyaya hizo hazikuwa zimechunika sehemu yoyote wala kuwa na dalili ya hitilafu.
Source;millardayo!

Saturday, May 2, 2015

ALI KIBA AVAMIWA NYUMBANI KWAKE JIJINI DAR.


IMG-20150502-WA0007
     

IMG-20150502-WA0002


IMG-20150502-WA0000


IMG-20150502-WA0001


IMG-20150502-WA0003

Usiku wa kuamkia leo msanii Ali Kiba akiwa nyumbani kwake Kunduchi jijini Dar-es-salaam, amevamiwa na kundi la watu wapatao 15 wanaodhaniwa kuwa ni majambazi.
Watu hao waliokuwa na silaha za aina tofauti yakiwemo mapanga,visu na silaha za moto walifanikiwa kuvunja milango na kuingia ndani kisha kuwadhuru baadhi ya ndugu wa ali kiba na kuiba mali pamoja na kila kitu walichoweza kubeba.
   Baada ya abdu kiba kuhojiwa alisema kwamba yeye alikuwa masaki, Ali akampigia simu kwamba kuna watu kama 15 hivi wamevamia nyumbani kwao. Waliovamia waliruka ukuta saa tisa za usiku, wakavunja mlango wa sebuleni, wakawakuta vijana wawili ambao wanaishi nao, waliwapiga na kuwalazimisha waoneshe chumba ambacho Ali kiba yupo. Wale vijana wakajibu kwamba ali hayupo wakauliza chumba chake wakaoneshwa chumba cha Abdu kiba. 
    Wameingia chumbani wakamkosa Ali kiba, wameiba vitu vingi vya sebuleni na chumbani pia pamoja na pesa milion 2 na nusu zilizokuwa chumbani kwa Abdu kiba.
Abdu kiba akatoa taarifa polisi, wakafika usiku huo huo na kuanza ukaguzi eneo lote la nyumba,
Da! inasikitisha sana kwa taarifa hizi!..

Sunday, April 26, 2015

MO MUSIC - NITAZOEA NEW MP3 DOWNLOAD.


                                               
                                                        Mo music-Nitazoea mp3

                                          Download